RSS Feed

FETTY AND FRIENDS

FURAHIA MIZIKI YETU


Myspace music player

Wednesday, March 7, 2012

NENO KUTOKA UBELGIJI KWA ABDUL WA MAISHA PLUS





Home is where my heart resides.....
Watanzania wenzangu, tumshukuru muumba kwa kutujalia nchi nzuri yenye
amani na utajiri wa maliasili ambao tumeajliwa.
Tuliombee pia taifa liondoke katika shida ya migomo, mafisadi, mgao wa
umeme, magonjwa, maafa na taabu zote za dunia.

Haijalishi nipo wapi sasa hivi, my heart is at home.
MUNGU IBARIKI TANZANIA

Monday, March 5, 2012

MKE WA PEDESHEE AMVAA WEMA KWEUPEEE

Muigizaji maarufu nchini Wema Sepetu avamiwa na anaesemekeana kuwa ni mke wa pedeshee anaetembea nae jana jioni maeneo ya kinondoni. Mwana mama huyo alifika katika baa yake na kumkuta wema na wasanii wenzake wa movie wakijaribu kuondoka, ndipo akaanzisha sakata na kuanza kuligonga gari la
 wema kwa maksudi kwa kutumia gari lake la kifahari aina ya range mara tatu mfululizo na kuliacha gari la wema linalosemekana ni la mwana mama huyo ambalo wema alihongwa na pedeshee huyo..
kesi iko oysterbay polisi kwa habari zaidi......stick na blog yako ya kijanja

TAARIFA YA MSIBA KUTOKA KATIKA FAILIA YA BWANA GABRIEL MPONZI WA OYSTERBAY



Familia ya Bwana Gabriel Mponzi wa Oysterbay,Jijini Dar-es-salaam.Wanasikitika kutangaza kifo cha mpendwa mtoto wao Jane Mponzi “Mama Melanie” pichani kilichotokea siku ya jumapili tarehe 4/3/2012 katika Hospitali ya Agha Khan Dar-es-salaam.

Ibada ya kumuaga marehemu itafanyika Jumanne tarehe 6/3/2012 nyumbani kwa marehemu Oysterbay, Dar-es-salaam kuanzia saa 6 mchana na marehemu atazikwa Ipamba-Tosamaganga, Iringa siku ya Jumatano tarehe 7/3/ 2012.

Kwa maelezo zaidi kuhusu ratiba ya mazishi, wasiliana na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Dr. Ponziano Mponzi kupitia namba 0767 600 604.
Ndugu, jamaa na marafiki waliopo mbali, wanaweza kutuma michango yao ya kufanikisha safari ya mwisho ya kwenda kumlaza mpendwa wetu Iringa kupitia:

M-PESA- 0756 -999-900

TIGO PESA- 0713 -123- 617

AIRTEL MONEY- 0784- 615-566

Bwana ametoa na Bwana ametwaa,Jina la Bwana lihimidiwe.

Amina.

KUONA TAMASHA LA PASAKA 2,000

kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kushuhudia onesho la tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika Aprili 8 mwaka huu, watalazimika kulipa kiingilio kidogo cha sh. 2,000 na sh. 5,000 kwa viti vya kawaida.


Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama wa Kampuni ya Msama Promotions, alisema Dar es Salaam leo kuwa wametenga viingilio katika kategoria tatu tofauti. Msama alisema watoto watalipa sh. 2,000, mashabiki watakaokaa viti maalumu watalipa sh. 10,000 na watakaokaa viti vya kawaida watalipa sh. 5,000, na tiketi za kategoria zote hizo zitauzwa mlangoni.

Alisema tiketi za viti maalumu watakaohitaji wanaweza kupiga simu selula 0713 383838, 0786 383838 na 0786 373737 ili kupata tiketi na maelezo kinagaubaga. "Tumeamua kuweka kiingilio kidogo cha wastani ili kila mmoja apate fursa ya kushuhudia tamasha la Pasaka wakiwamo watoto," alisema Msama.
Msama alisisitiza kuwa tamasha hilo litahudhuriwa na wageni mbalimbali waalikwa kutoka ndani na nje ya nchi. Alisema tamasha hilo lina lengo la kuchangia watoto yatima ambao wazazi wao wamefariki kwa ugonjwa wa ukimwi na mitaji ya wanawake wajane wasiojiweza.
Fedha zilizopatikana katika tamasha la mwaka jana zilitumika kuwasaidia waathirika wa mabomu yaliyotokea katika kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Gongo la Mboto, Dar es Salaam na pia kuwapa mitaji wajane wasiojiweza. Baadhi ya wasanii wa nyimbo za Injili waliothibitisha kupamba tamasha hilo mwaka huu ni Upendo Kilahiro, Upendo Nkone, Atosha Kissava na kundi la Glorious Celebration.

Mbali na Dar es Salaam, tamasha la Pasaka pia litafanyika mjini Dodoma Aprili 9 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri ambayo ni Jumatatu ya Pasaka. Tamasha la Pasaka la mwaka huu pia litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi sita za Afrika ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Afrika Kusini na Zambia. Pia kutakuwa na kwaya.

Friday, March 2, 2012

STEREO NA FID WAKITOA MA FREESTYLE PART 1 & 2




STEREO ATANGAZA KUJITOA LUNDUNO

FID Q AKIACHIA FREESTYLE LEO HII NDANI YA XXL MICHANO CRAZY FRIDAY


KAMPUNI Y AMAWASILIANO YA ETISALAT YASHINDA TUZO 3 ZA KIMATAIFA

Etisalat Group Chief Commercial Officer and Zantel's Chairman Essa Al Haddad (right) poses with one of the 3 awards Etisalat won for its innovative products in m-health and mobile money in the GSMA Awards held recently in Barcelona Spain. With him are Etisalat Group CEO Ahmed Abdul Karim Julfar (centre) and Etisalat Group Senior Director Products and Services George Held.
Huduma yake ya Mobile Baby yanyakuwa tuzo 2 wakati huduma yake ya malipo kwa kutumia simu yapewa tuzo ya ubunifu
Kampuni ya mawasiliano inayoongoza Mashariki ya Kati, bara la Afrika na Asia imefanikiwa kuonyesha umahiri wake kwenye sekta ya mawasiliano kwa kunyakuwa tuzo 3 kwenye kongamano la mawasiliano linalofanyika kila mwaka Barcelona, Uhispania. Tuzo mbili ni za huduma yake ya ‘Mobile Baby’ ambayo inatoa huduma za afya kwa njia ya simu na tuzo ya tatu ni kwa ajili ya huduma bunifu ya kufanya malipo ya kiasi chochote kwa njia ya simu wakitumia teknologia mpya ijulikanayo kama Near Field Communications (NFC).
Makamu Rais wa Kibiashara Etisalat na Afisa Mkuu wa Kibiashara wa Zantel Ahmed Mokhles alisema ushindi huu ni ishara ya ahadi zake kwa wateja wake kuwa wabunifu kila mara kupitia huduma na bidhaa zake. “Kampuni ya Etisalat imewekeza sana katika teknologia ikiwa na lengo la kubadilisha sura ya sekta ya mawasiliano na inaheshimika duniani kote kwa ubunifu wa bidhaa na huduma zake. Kila mara inakuja na vitu vipya na pekee vinavyobadilisha maisha ya jamii. Kupitia huduma hizi mbili zilizoshinda tuzo tumefanikiwa kufanya hivyo kuleta huduma karibu na jamii kwa muda unaofaa, kwa njia salama na ufanisi mkubwa.” alielezea Bw. Mokhles.
Huduma ya Mobile Baby ni ushirikiano na kampuni ya Qualcomm, D-Tree International pamoja na Great Connection inasaidia kutoa huduma za afya haswa kwa waliyo mbali na huduma za afya na tangu ianzishwe mwaka jana imeonyesha matokeo ya kuridhisha katika kutimiza lengo la millennia la 5 ambalo ni lupunguza vifo vya kina mama na watoto kwa asilimia 75 na kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwa wote kufikia mwaka 2015.
Huduma ya Mobile Baby inafanya kazi hivi: Muhudumu wa afya/mkunga kupitia simu yake ya mkononi hujaza eneo alipo, kituo cha afya kilichopo karibu pamoja na taarifa za muuguzi na dereva aliye karibu. Kupitia huduma hii muhudumu wa afya ataweza kuingiza taarifa za maendeleo ya akina mama wajawazito wa eneo lake ambao wamejiandikisha kwenye program hii. Muhudumu pia atawasaidia akina mama kujifunguwa na ataweza kuwasiliana na madaktari kwa njia ya simu kuhakikisha anazingatia kanuni za uzazi salama. Wakati wa dharura ataweza kumsafirisha mama hadi kituo cha afya kilichopo karibu na kulipia usafiri kupitiaa huduma ya pesa kwenye simu Ezy Pesa. Huduma hii ilianzishwa kwanza Tanzania mwaka jana mwezi wa tisa kupitia mtandao wa Zantel na takwimu zinaonesha kwamba kumekuwa na punguzo la asilimia 30 la vifo vya akina mama na watoto.
Mafanikio ya huduma ya Mobile Baby nchini Tanzania, Nigeria, Milki za Kiarabu na Afrika Kusini Etisalat ina mpango wa kuanzisha huduma hii kwenye mashirika yake mwaka huu wa 2012 nchi zifuatazo Afghanistani, Pakistani, Sri Lanka, Ivory Coast, Benin, Togo, Niger na Gabon.

PADRI APONGEZA KUFANYIKA KWA TAMASHA LA PASAKA UWANJA WA TAIFA FEB 8




WADAU nchini wametakiwa kuiunga mkono Kampuni ya Msama Promotions kwa kuandaa matamasha ya Pasaka, yenye lengo la kusaidia matatizo mbalimbali katika jamii.

Kauli hiyo imetolewa leo na Padri wa Kanisa Katoliki Jimbo jipya la Ifakara, Deogratius Kisweka alipozungumza na Jambo Leo kwa njia ya simu.

Padri Kisweka alisema kitendo kinachofanywa na Kampuni ya Msama Promotions chini ya Mwenyekiti wake, Alex Msama ni cha kupongezwa.

Alisema kila mtu Mungu amempa kipawa chake, hivyo kitendo cha Msama kuandaa matamasha ya injili na kusaidia wajane wasiojiweza, yatima pamoja na kutoa baiskeli kwa walemavu ni jambo la kumshukuru Mungu.

"Ni watu wachache ambao wanaweza kufanya kama kinachofanywa na Msama, naamini kila mtu mwenye mapenzi mema anastahili kuunga mkono kwa kuhudhuria tamasha hilo," alisema Kisweka.

Pamoja na hilo, Padri huyo aliiomba Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo kutanua wigo kwa kulipeleka katika kila mikoa ili kutoa nafasi kwa wengine kuchangia.

Tamasha hilo linatarajiwa kurindima Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Aprili 8 mwaka huu na pia litafanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 9 mwaka huu.

Tayari kundi la muziki wa Injili la Glorious Celebration Spirit of Praise 'Gospel Live' linalotamba na albamu ya Niguse, limethibitisha kushiriki tamasha la Pasaka.

Msama alisema mbali na Glorious, waimbaji wengine waliothibitisha kushiriki mpaka sasa ni Upendo Kilahiro, Upendo Nkone na Atosha Kissava kutoka Mkoa wa Iringa.

Mbali na Tanzania, pia kutakuwa na waimbiaji kutoka Kenya, Uganda, Zambia, Afrika Kusini, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika tamasha hilo la nyimbo za injili za kumsifu Mungu.

Thursday, March 1, 2012

LIKE MOTHER LIKE DAUGHTER

Lulu akiwa bibi  pamoja na mama yake

WALISEMA CHABO NDIO YENYEWE..KWI KWI KWIII

KUTANA NA BUIBUI MWENYE NGUVU ZA KUMFANYA NYOKA KITOWEO CHA ASUBUHI

receptionist alifika ofisini kwake Bloemfontein, South Africa, na kukutana na hiki (pichani) karibu na meza yake . nyoka akiwa kazungushwa kwenye nyuzi za buibui huku akijisogeza kwa ajili kuanza kukifanya kitoeo.
cha kushangaza zaidi nyoka huyo alikuwa kasha nyayuliwa kutoka chini na kuning'inia ndani ya nyuzi hizo
huku buibui akimalizia kazi ndogo ya kujizungunsha kwa ndani kukipiga kitoeo hicho kilichomzidi mwili


PATA NAKALA YA GAZETI LAKO LA DIRA KWA HABARI ZILIZOCHAMBULIWA KWA KINA KWA SH 500 TU


BAADA YA KUPATA UMAARUFU KWA KUCHANA WIMBO WA NIKKI MINAJ .SOPHIA GRACE NA ROSIE WAMERUDI TENA



baada ya kupata umaarufu mkubwa kwa kuchana wimbo wa niki minaj SUPPER BASE kupitia youtube na kufanya interview na mwana mama Elen, Sophia Grace na Rosie wamechukua hatua nyingine kwa kutunga na kurekodi pini lao linalokwenda kwa jina la Disneyland

watu wakadhani hawawezi kuwashangaza tena now here they are na wimbo wa Kery Hilson



na sasa wamekuja na single yao mpya waliotunga na kurecord unaoitwa disneyland
Elen aliwapatia mabegi mawili fully na trip ya kwenda Disneyland

KIBAKA ACHOMWA MOTO MCHANA KWEUPEE

Jana mchana kijana ambae hakufahamika kwa jina alichomwa moto maeneo ya victoria kwa kairuki  kwa tuhuma za wizi wa pikipiki

PINI JIPYA: ARUSHA BILA VISU INAWEZEKANA / WATENGWA



JIUNGE NAMI KWENYE UPANDE WA EMAIL AU SIO