Mambo Vipi Guys.
Nimecheki website yenu na imenivutia sana. Mimi nahusika na mambo ya
production na ni shabiki mkubwa wa local music. Tafadhali Naomba
munipe nafasi nichangie maoni yangu kuhusu hii industry.
Siku hizi kuna malalamishi mengi ya wasanii kuhusu nyimbo zao kuibiwa
au albamu kuzuiwa na wasambazaji.Kwa sababu hiyo kunahitajika
mabadiliko makubwa ikiwa tunatarajia kuokoa industry hii.
Kunahitajika extensive surgery sehemu 3 muhimu:
RECORD LABEL
Inatakiwa kuanzishwa record label ambazo zitafanya kazi kama
makampuni. Sio studio kuwa label. Kampuni zikianzishwa kama record
label malengo yao yatakuwa ni kusaka vipaji, publicity za wasanii wao
na muhimu zaidi ni mauzo ya bidhaa zao (wasanii). Itakuwa hakuna haja
ya wasanii kujihusisha na wasamabazaji tena. Ikiwa label wamewekeza
kwa wasanii watahakikisha yakuwa bidhaa zao hazitaibiwa au kuhujumiwa.
Watakuwa na uwezo wa kutumia vyombo vya sheria na msanii atafaidika.
MUSIC PUBLISHERS
Kuna haja ya kuanzisha music publishing companies kuwa wakala wa
composers wa nyimbo na mashairi. Publishers wanakuwa kama soko la
record labels kununua nyimbo ambazo zinaweza kuwatoa wasanii wao. Kuna
wengi wana vipaji vya kutunga mashairi au melodies na songwriting
(composers) na kuna wasanii wengi wana vipaji vya kuimba lakinio sio
kutunga.Composers wanaweza kuwapa publishers nyimbo zao na publishers
watatafuta soko. Kutakuwa na mikataba ya kisheria baina yao na kila
mtu atafaidika kwa njia hiyo. Mipango hii ipo haswa nchi
zilizoendelea. Kwa wasanii wengi nyimbo wanazoimba Record label ndiyo
iliyo nunua naye akatia sauti yake. Njia hii itaweza kubuni ajira kwa
wengi.
DISTRIBUTION
Siku hizi kwenye vyombo vya habari tetesi kubwa ni kuhusu wasambazaji
wa muziki. Hili tatizo linasababishwa na albam mpya kuw nyingi na
mikataba duni. Kwa miaka mingi wasmbazaji ni wale wale. Hawawezi
kukidhi mahitaji ya soko. Kazi nyingi zinachelewa kuingia sokoni na
upande mwengine wasanii wanapewa dili ambazo hazifai. Ni wakati
muafaka kwa makampuni mengine kuingia biashara hii.
Pili kwa bidhaa zinazoingia sokoni ni vizuri kuwe na system ya kuzipa
Registration code ambayo itakuwa na Bar code maalum ili kujua hesabu
za bidhaa zilizozalishwa. Na Record label zilipwe kutegemea na bidhaa
zilizozalishwa sio zilizouza sokoni. Namba hizi maalum zitasaidia hata
serikali kukadiria kodi yake na pia kukagua bidhaa feki sokoni.
WASANII
Wasanii nao wanafaa kujihusisha na the other side of the music
business. Hii ni kama vile kuelewa mikataba na majukumu yao ndani ya
mikataba wanayoingia na Record labels,promoters au sponsors. Everytime
wajitahidi kuboresha kazi zao na muhimu zaidi ni kufanya kazi kwa
bidii na kujitolea (commitment). Malengo yao yawe kufikia masoko mengi
zaidi duniani.
COSOTA
Cosota wanahitajika kuongeza nguvu katika kukusanya royalties.
Wazilazimishe radio na TV stations kuwa na playlist ya kila siku
ambayo itatumika kujua nyimbo zipi zilizochezwa na kukusanya
royalties. Pia wanahitajika kuongeza kwenye listi yao sehemu zengine
za kukusanya kama vile video halls, daladala, ma saloon, clubs na bar.
Sehemu yoyote ya biashara ambapo muziki au hata redio inatumika
kuvutia wateja wanatakiwa walipe. Walipishwe kiasi kidogo kwa mwaka.
Hii itaongezea kipato kwa wasanii. Kuwe na music copyright inspectors
ambao wanauwezo wa ku enforce sheria hizi. Jeshi la polisi linafaa
kuwa na kitengo maalum cha anti piracy.
Haya ni maoni yangu binafsi kwa uchache.
Mahamud Omari