SIKILIZA BONGO FLAVA MPYA HAPA


fetty
Quantcast

JIUNGE NAMI KWENYE UPANDE WA EMAIL AU SIO


fetty
Quantcast

Thursday, November 12, 2009

KAMA SIJAELEWA HIVI .......


mkono wa mwanadada nakaaya sumari na tatoo ya ukweli ikisomeka jina la mchizi kutoka kundi la dead prezz M I ambae miezi kadhaa iliyopita alimuingeji



lakini kwa sasa tatoo hiyo inasomeka hivi (n na ramani ya africa) ile ( 1 ) ikiwa imefutiliwa mbali, hapa ndipo maswali yakifatiwa na mshangao mkubwa yanajaa akilini mwangu sasa sielewi!!!!!!!!kama weiye wafahamu tupe maoni yako mazee.

Wednesday, November 11, 2009

HASHEEM THABIT AVUNJIKA TAYA


Mchezaji wa kati wa timu ya Memphis Grizzlies Hasheem Thabeet amevunjika taya lake la chini siku ya jana, alipokuwa akichezea na timu yake wakiminyana na Portland Trail Blazers, mchezo amabo ulimalizika kwa Blazers kutoka na ushindi wa pointi 93 kwa 79.

Hii sasa inamaanisha kuwa Hasheem hatokuwemo kwenye msafara wa timu yake ya Grizzlies itakapokuwa ikienda kucheza na Houston Rockets usiku wa leo.

Hata hivyo habari si mbaya sana za kuumia kwake kwani baada ya uchunguzi wa madaktari imefahamika kuwa, hatohitaji upasuaji, ili kutibu maumivu na wakasema anatarajiwa awe amepona si muda mrefu sana kuanzia sasa, na ni wazi kuwa hii ni taarifa njema ambayo Thabeet atakuwa amefurahishwa nayo, timu yake na Watanzania kwa ujumla.

Tuesday, November 10, 2009

CHEKI NA VIDEO YA DIAMOND/ KAMWAMBIE


diamond ni mmoja kati ya wasanii wapya wanaotarajiwa kufanya vizuri sana siku za mbele ni single yake ya kwanza na inafanya vizuri sana katika upande wa video kupitia boda2boda ya tbc 1 inaitwa kamwambie.BIBI UNAEMUONA HAPO MWISHONI NI BIBI YAKE NA DIAMOND NA AMEFARIKI JUMAMOSI YA TAREHE 7/11/2009. MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI... AMEN

IBUA FILMS STAR TANZANIA YAHAMIA MWANZA


majaji wakishoo love na madeni kutoka a-town

Baada ya mchakato mzima wa kuibua vipaji vya wasanii chipukizi wa maigizo yaani IBUA Film Star Tanzania kuanzia Arusha, zoezi zima linahamia Mwanza katika Nyanza Shule ya msingi iliyopo Balewa Road tarehe 14 na 15 Novemba kabla ya kuhamia Dodoma.

Chipukizi waliofanikiwa kuiwakilisha mkoa wa Arusha ni pamoja na Salum Ahmed Shafii, Pauline Edward Munisi, Michael Elias Mrema, Mbara Meena na Enhard Haruna. Kutokana na mwamko mkubwa wa wasanii chipukizi, fomu za kujiunga na shindano la IBUA Film Star Tanzania zinaendelea kutolewa maeneo mbali mbali na mikoa husika. Hii ni kuwawezesha wasanii chipukizi
majaji akishow love na washirik

kupata nafasi ya kuonyesha uwezo wao ya kuendeleza vipaji vyao na kuviacha vikipotea kwa kukosa njia ya kuvikuza. Usaili wa mikoani utaandaliwa vipindi maalum na kuonyeshwa kupitia mojawapo ya runinga hapa nchini.

Taasisi ya YEC Production, inayojihusisha na kukuza na kuibua vipaji kwa vijana katika ulingo wa filamu nchini, imegundua njia pekee ya kuibua vipaji hivyo na kuviokoa visipotee kwa kuanzisha shindano maalum la kusaka vipaji. Washiriki wataonyeshwa kwenye runinga kupitia kipindi maalum ambapo watazamaji watahusishwa kumpata staa halisi wa filamu Tanzania.

Mbali na kuviendeleza vipaji vyao pia washiriki watapata mafunzo katika nyanja zote kuanzia za uandishi wa muongozo (scripting) hadi uigizaji bora na kuwawezesha kufikia malengo yao.

Vigezo vilivyotumika katika kumsaka msanii huyo chipukizi ni kuwa na umri wa miaka 16 ikiwa ni pamoja na uelewa. Hata kutokuonekana katika tamthilia au sinema ya aina fulani hapa nchini hicho pia ni kigezo kimojawapo ambacho ni kizuri, kwani vijana wanaochipukia ndiyo wanahitaji msaada mkubwa katika kuibuliwa vipaji, tofauti na wakongwe ambao tayari wamejitangaza.

YEC, imeahidi kuyaangalia matatizo yanayowakabili wasanii kwa kina na kuahidi kutoyarudia, kama yanavyofanywa na baadhi ya wasanii wakongwe, ndiyo maana wameamua kuingia mikataba ya mwaka mmoja na washindi watakaofika kumi bora, ili kuliepuka tatizo hilo.

ALBUM YA NGWEA KWENYE KONA KUINGIA SOKONI


album ya mtu mzima mwenye sur name ya freestyle Ngwea,a.k.a mimi inayoitwa NGE (nyota yake) ikiwa na mwaka aliozaliwa 1982 kwenye poster unayoiona hapo juu itaingia sokoni sio muda mrefu.

MKALI WA ZOUK KUTOKA IRINGA



WAKALI WA ZOUK TANZANIA MPO TAYARI? Msanii mpya wa mahadhi ya ZOUK
anayekuja juu kwa kasi ya ajabu zaidi ya kimbunga cha TSUNAMI,ni zao
jipya kutoka Nyanda Za Juu Kusini nazungumzia wilaya ya Njombe ndani
ya mkoa wa IRINGA ni msanii anayejulikana kwa jina la kisanii AMANI
WETU jina lake halisi ni AMANI SAID KILLO,anaingia kwenye ulingo wa
Zouk akijitambulisha na wimbo wake mpya uitwao 'MAPENZI NI ZAWADI'
ikiwa ndio maandalizi ya Album yake ya kwanza itakayo kwenda kwa jina
la MOYO FICHO LA SIRI.mpaka sasa amesharekodi nyimbo nne katika studio
ya SOUND POWER chini ya Producer B jayzee(THE PROVIDER) studio hiyo
ipo Njombe mjini.Mpaka sasa kazi ambazo amesharekodi ni pamoja na
MAPENZI NI ZAWADI,RAFIKI,MOYO FICHO LA SIRI na WAUZA SURA na kazi
nyingine mpya inayopikwa jikoni kwasasa inaitwa NIMEMPATA,Hivyo
anaomba wapenzi wa muziki wa Zouk wakae tayari kwani mwanzoni mwa
mwaka 2010 album yake itakuwa sokoni

Monday, November 9, 2009

BABA MZAZI WA MANDOJO AMEFARIKI DUNIA


baba mzazi wa mandojo wakwanza kutoka kushoto anaejulikana kama francis michael ongoso amefariki dunia leo hii na mazishi yatafanyika kwao Manyoni Singida.MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEM MAHALI PEMA PEPONI,,, AMEN

MAISHA CLUB KWISHAAAA ...YATEKETEA KWA MOTO

sehemu kuu ya burudani Maisha Club iliyopo Masaki jijini Dar leo mnamo majira ya saa saba mchana ilianza kuwaka moto, kwa taarifa zilizopatikana kutoka kwa mashuhuda wamesema kuwa kulikuwapo na ukarabati uliokuwa unaendelea wa vipupwe (AC), kwa bahati mbaya wakati wa ukarabati huo mojawapo ikalipuka kutokana na nyaya zake kugusana, na baadaye moto mkubwa ukazuka katika jengo hilo, imeelezwa kuwa taarifa zilifika kwa watu wa zima moto lakini hawakuwahi kuuzima moto huo kwa haraka kwani kwa asilimia kubwa vitu vilivyokuwemo vilikuwe vimekwishateketea.

hii ndio ilikuwa sehemu ya kuingilia maishani

sura ya mbele ya club maisha kulia ndipo swiming pool ilipo

maisha club inavyoonekana baada ya kuwaka moto

Thursday, November 5, 2009

FIESTA ONE LOVE LASOGEZWA MBELE


Tamasha la Fiesta One Love 2009 lililotarajiwa kufanyika jumamosi hii,Novemba 7 katika uwanja wa posta,kijitonyama jijini Dar,limeaihirishwa na kusogezwa mbele.


Akizungumza mratibu mkuu wa tamasha hilo Bw.Ruge Mutahaba amesema kuwa tamasha hilo limeaihirishwa hadi Novemba 21,mabadiliko hayo yanatokana na wahusika wakuu wakiwemo wafanyakazi wa Clouds Media Group/Prime Time Promotions (ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo waandaji wa tamasha hilo) kuondokewa (kufariki) kwa Mwenyekiti wao Mzee Alex Mkama Kusaga juzi jioni nchini Afrika ya Kusini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu.


Mutahaba amesema ratiba ya wasanii wambao walipaswa kushiriki kwenye tamasha hilo la Kitaifa iko pale pale wala haijabadilika,na kwamba msanii ambaye alitajwa angewatumbuiza wakazi wa Dar kutoka chini Marekani kwenye tamasha hilo,Buster Rhymes na wenzake naye ratiba yake iko pale pale,kwamba atakamua vilivyo siku hiyo. .
Aidha kwa taarifa za msiba wa Mzee K. inaelezwa kuwa mwili wake utawasili leo jioni na msiba upo nyumbani kwake Mbezi Beach karibu na Girrafe Hotel,kuhusu ratiba za mazishi na mambo mengine tutaendelea kufahamishana zaidi.

HIPPO DANCE FIESTA ONE LOVE ANIMATION


ANIMATION KUTOKA TANZANIA KUPROMOT FIESTA ONE LOVE 2009, TAMASHA KUBWA LA MUZIKI NCHINI TANZANIA NA AFRIKA MSAHARIKI NZIMA.LINALOANDALIWA NA CLOUDS ENTERTAINMENT CHINI YA UDHAMINI WA SERENGETI LAGER, NOKIA,ZAIN AND TACAIDS.IMEFANYWA NA EDWIN A.K.A BIGGIE AU SABA SITA KUTOKA CLOUDS TV.

Wednesday, November 4, 2009

NGOMA MPYA BLOGUNI....


mtoto wa kitanzania anaewakilisha jiji la tanga Roma ametoka na ngoma mpya inayoitwa MR PRESIDENT watu walishaizungumzia sana makali ya meseji iliyo katika ngoma hii. ney pia ametoka na ngoma mpya inayoitwa JINSI, baada ya kupata air play yakutosha ngoma yake inayoitwa itafahamika tu.ZISIKILIZE HAPO JUU

MWENYEKITI MTENDAJI WA CLOUDS MEDIA GROUP AFARIKI DUNIA


Mwenyekiti mtendaji wa Clouds Media Group,Bw Alex Kusaga ambaye ni baba yake mzazi na Joseph Kusaga, amefariki leo alasiri (jana) Pretoria ,nchini Afrika ya Kusini ambako alipelekwa kwa ajili ya matibabu.


Kwa taarifa zilizopatika ni kwamba msiba upo nyumbani kwake Mbezi-Beach karibu na Giraffe Hotel.


Aidha kwa taarifa zaidi tutaendelea kufahamishana kadiri ya zitakavyokuwa zinatujia.


MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMEN

Saturday, October 31, 2009

WASANII NA WASHABIKI WA BONGO FLEVA INAWAHUSU ZAIDI

Mambo Vipi Guys.

Nimecheki website yenu na imenivutia sana. Mimi nahusika na mambo ya
production na ni shabiki mkubwa wa local music. Tafadhali Naomba
munipe nafasi nichangie maoni yangu kuhusu hii industry.

Siku hizi kuna malalamishi mengi ya wasanii kuhusu nyimbo zao kuibiwa
au albamu kuzuiwa na wasambazaji.Kwa sababu hiyo kunahitajika
mabadiliko makubwa ikiwa tunatarajia kuokoa industry hii.

Kunahitajika extensive surgery sehemu 3 muhimu:

RECORD LABEL
Inatakiwa kuanzishwa record label ambazo zitafanya kazi kama
makampuni. Sio studio kuwa label. Kampuni zikianzishwa kama record
label malengo yao yatakuwa ni kusaka vipaji, publicity za wasanii wao
na muhimu zaidi ni mauzo ya bidhaa zao (wasanii). Itakuwa hakuna haja
ya wasanii kujihusisha na wasamabazaji tena. Ikiwa label wamewekeza
kwa wasanii watahakikisha yakuwa bidhaa zao hazitaibiwa au kuhujumiwa.
Watakuwa na uwezo wa kutumia vyombo vya sheria na msanii atafaidika.

MUSIC PUBLISHERS
Kuna haja ya kuanzisha music publishing companies kuwa wakala wa
composers wa nyimbo na mashairi. Publishers wanakuwa kama soko la
record labels kununua nyimbo ambazo zinaweza kuwatoa wasanii wao. Kuna
wengi wana vipaji vya kutunga mashairi au melodies na songwriting
(composers) na kuna wasanii wengi wana vipaji vya kuimba lakinio sio
kutunga.Composers wanaweza kuwapa publishers nyimbo zao na publishers
watatafuta soko. Kutakuwa na mikataba ya kisheria baina yao na kila
mtu atafaidika kwa njia hiyo. Mipango hii ipo haswa nchi
zilizoendelea. Kwa wasanii wengi nyimbo wanazoimba Record label ndiyo
iliyo nunua naye akatia sauti yake. Njia hii itaweza kubuni ajira kwa
wengi.
DISTRIBUTION
Siku hizi kwenye vyombo vya habari tetesi kubwa ni kuhusu wasambazaji
wa muziki. Hili tatizo linasababishwa na albam mpya kuw nyingi na
mikataba duni. Kwa miaka mingi wasmbazaji ni wale wale. Hawawezi
kukidhi mahitaji ya soko. Kazi nyingi zinachelewa kuingia sokoni na
upande mwengine wasanii wanapewa dili ambazo hazifai. Ni wakati
muafaka kwa makampuni mengine kuingia biashara hii.

Pili kwa bidhaa zinazoingia sokoni ni vizuri kuwe na system ya kuzipa
Registration code ambayo itakuwa na Bar code maalum ili kujua hesabu
za bidhaa zilizozalishwa. Na Record label zilipwe kutegemea na bidhaa
zilizozalishwa sio zilizouza sokoni. Namba hizi maalum zitasaidia hata
serikali kukadiria kodi yake na pia kukagua bidhaa feki sokoni.

WASANII
Wasanii nao wanafaa kujihusisha na the other side of the music
business. Hii ni kama vile kuelewa mikataba na majukumu yao ndani ya
mikataba wanayoingia na Record labels,promoters au sponsors. Everytime
wajitahidi kuboresha kazi zao na muhimu zaidi ni kufanya kazi kwa
bidii na kujitolea (commitment). Malengo yao yawe kufikia masoko mengi
zaidi duniani.

COSOTA
Cosota wanahitajika kuongeza nguvu katika kukusanya royalties.
Wazilazimishe radio na TV stations kuwa na playlist ya kila siku
ambayo itatumika kujua nyimbo zipi zilizochezwa na kukusanya
royalties. Pia wanahitajika kuongeza kwenye listi yao sehemu zengine
za kukusanya kama vile video halls, daladala, ma saloon, clubs na bar.
Sehemu yoyote ya biashara ambapo muziki au hata redio inatumika
kuvutia wateja wanatakiwa walipe. Walipishwe kiasi kidogo kwa mwaka.
Hii itaongezea kipato kwa wasanii. Kuwe na music copyright inspectors
ambao wanauwezo wa ku enforce sheria hizi. Jeshi la polisi linafaa
kuwa na kitengo maalum cha anti piracy.


Haya ni maoni yangu binafsi kwa uchache.

Mahamud Omari

ZIZZOU ENTERTAINMENT SASA NI HISTORIA KWA BUSHOKE


baada ya kutoka na album moja iliyokuwa na mafanikio akiwa chini ya lebo zizzou yaani zizzou entertainment, bushoke hayuko tena chini ya lebo hiyo.jana nilipata nafasi ya kuongea na mkuu mwenywe tippo amesema,bushoke hayupo tena katika lebo yangu na badala yake nimemsaini legendary zahir zoro ambae ni baba wa wanamuziki wawili wanaofanya poa pia katika gemu nawazungumzia maunda na banana zahir zoro.

Friday, October 30, 2009

WAZO LA MDAU JAMANI TUPENI MAONI

Hi fetty,op ur doing great mdada,
Ee bwana nimesafiri kikazi mkoa wa Singida sa unajua tena kila mtu anastarehe zake na club ndo nguzo ya starehe za watu wengi even you,bt mkoa huu wa Singida nimeona tofauti na pande zote za Tanzania fetty.Hapa Singida kuna ukumbi mmoja tu wa disco unaoitwa Metro au Pamba disco,Bt cha kushangaza ni pale nlipozama club nkiwa na washkaji nikawaona watu wenye bunduki sio kwa kujificha hapana bt zikiwa begani,Bt fetty nliduwaa mbaya nlifkiri club imevamiwa kumbe ni polisi wanatoka lindoni wakifika mlangoni wanatema bit kwa wale wa mlangoni na kuingia na bunduki zao sa jamani fetyy najiuliza maswali 4,Ikitokea bahati mbaya itakuaje?Kutokana na kwamba wanakunywa na pombe akilewa mmoja wao hawezi kuua mtu?Je serikali haina sheria jamani?Je polisi hawazijui sheria?na je uongozi wa hiyo metro club haujui ni kosa kumruhusu mtu kuingia na bunduki disco?Fetty i went there twice na wananchi wanakiri ndo kawaida ya baadhi ya polisi wa Singida kuacha lindo na kuja club sa hadi na GUN?Yaani imenikera na nawadissssssss mbaya ile mbaya wajue kuwa sio issue wala nini maana anything can happen.Ni hayo tu mdafada.bt nkienda tena ill send u snap zao 4 confirmation
Its mbimbwa (Operating manager smwhere)

Thursday, October 29, 2009

MR 2 KUWASHA MOTO BONGO DAR ES SALAAM


mr 2 aka sugu (joseph mbilinyi) anatarajia kuuwasha moto ndani ya diamond jubilee katika mkesha wa xmass.

Wednesday, October 28, 2009

WAPI WIKI HII...MPANGO MZIMA.KAZI KUDHIBITI KAZI


Karibuni kwa mara nyingine tena, husika na WaPi ...tamasha la kila mwezi. Kama kawaida"WaPi" inaendelea kwa muundo wa kila miezi mitatu. Baada ya mzunguko wa mikoani..Iringa mwezi wa 8-08-09, Arusha 3-10-09.

Tumerejea Daa. Safari hii kauli mbiu yetu ni Mpango Mzima... kwenye mada yetu "MPANGO MZIMA...kazi kudhibiti kazi"... KIJIWE MAARIFA tutakuwa na Boyd Oyier msanii mahiri wa uchoraji na usanifu taswira. Atafanya warsha ya uchoraji, usanifu wa taswira


Yawaletea

Nyota kali (mziki asilia), Wakwetu (motherland), Young-D(msanii chipukizi wa rap), Maya(mshairi), Msafiri Zawose, Momo (msanii wa hiphop toka Canada), Tafakari emsii mahiri chipukizi), Manzii(msanii wa hiphop toka Rwanda) Wasanii mbali mbali wa sauti ya handaki(undeground), Katika harakati.

Madijei, ma emsii, machata, mabreka ,michoro mbali mbali, ushairi,ngoma, maigizo na usanifu mitindo.

Mahali: British Council, Dar Es Salaam


(maelekezo: Samora na Ohio, mkabala na Steers kati kati ya jiji)


Jumatano, 31-10-2009 mida; saa 9 -alasiri-hadi 2 usiku
Mada ya mwezi:ni MPANGO MZIMA-kazi kudhibiti kazi

CHEKI NA VIDEO YA O.C.G


angalia video mpya ya o.c.g inayoitwa rafiki ambayo ameifanya akiwa finland beat ikiwa ya mtu mzima mika mwamba. o.c.g alishawi kutoka na ngoma yake inayoitwa agwelina kipindi alichokuwa bongo

Tuesday, October 27, 2009

OPINI JIPYA BLOGUNI


mkongwe wa ladha za kibongo mr 2 ametoa ngoma mpya inaitwa HOLD ON isikilize hapo juu

ONE LOVE NDANI YA JIJI LA MAPENZI TANGA FIESTA 2009


anawakilisha ilala lafamili chi chi chi chi chiiiiiii chidi beenz na mkuu wa kundi chiku ketto

tuko high kama klm

fredy akipiga za ki legendary wa pop michael jackson

cheki na swaga za mzee wa ma bullet quick racka

ni moja kati ya familia iliyoenea muziki ndani ya damu zao kuanzia baba kaka na hata yeye mwenyewe muite maunda zorro akiimba nyimbo zake kali kama penzi la wawili, niwe wako na daladala

kutoka tht wanaitwa barnaba na pipi wanaokamata chati za muziki tanzania na pini lao linaloitwa NJIA PANDA.

vijana wa tanzania house of talent (tht) wakiikamua stage vizuri

nyomi hiloooooooooooo