SIKILIZA BONGO FLAVA MPYA HAPA


fetty
Quantcast

PIGIA KURA NGOMA YAKO KALI

JIUNGE NAMI KWENYE UPANDE WA EMAIL AU SIO


fetty
Quantcast

Wednesday, November 25, 2009

MDAU WA ZE BLOG


Mdau wa ze blog hii, Allen Sobo anawapa anawapa hi! wooote

Tuesday, November 24, 2009

WASHINDI WA FIESTA ONE LOVE KIMYA KIMYA



hawa ni baadhi ya wahindi wa fiesta one love kimya kimya ambao walijishindia zawadi kibao kutoka zain, nokia na serengeti ikiwa ni pamoja na pesa taslim kutoka Clouds Fm

HAPPY BIRTHDAY DINA MARIOS



bonge la keki unabishaaaaaaaaaaaa

Friday, November 20, 2009

FIESTA ONE LOVE 2009 REHESAL.....


stage la fiesta pne love 2009 linayoonekana kabla halijamaliza kutengenezwa jana usiku wasanii wote walikuwepo kwaajili ya rehesal

qj aliniambia sio kuimba tu hata nguzo mojawapo ya hiphop anaiweza pia



kutoka kushoto ni b12, fe'e na quick racka

mwanadafada baby madaha na maunda wakisubiri zam yao

Wednesday, November 18, 2009

MORRACA AJITOA RACKAS


the sexsiest men muite morraca
muasisi na muanzilishi wa kundi la rackas lenye vichwa vikali ndani nawazungumzia quick racka, chief racka na dowracka amejitoa katika kundi hilo kwasababu ambazo yeye mwenyewe hakuzisema.morraca amesema amejitoa kundini lakini sababu atazifafanua zaidi sio muda mrefu.utapata updates mara tu taarifa zitakaponifikia

kundi zima la rackars

Tuesday, November 17, 2009

MTOTO HUYU PIA HUTOKWA MACHOZI YA DAMU


hii sasa inaanza kama kushangaza baada ya kufikia watu watatu kuwa na tatizo hili la kutokwa na mchozi ya damu badala ya machozi ya kawaida (maji).mtoto huyu anaitwa TWINKLE ambae kwa hivi sasa anapata miaka mwili sasa.mtoto huyu hutokwa na damu utosini, kiganjani, miguuni, na machoni na sehemu zinginezo.

ATOKWA NA MACHOZ YA DAMU KILA ATOAPO MACHOZI



MWANAMKE nchini India, Rashida Khatoon, amekuwa gumzo nchini humo kutokana na hali yake ya kutoa machozi ya damu kila anapolia.Rashida amewashangaza hata madaktari kwa hali yake hiyo ya kutiririka machozi ya damu kila anapolia.
Kwa siku mwanamke huyo humwaga chozi la damu mara kadhaa."Sisikii maumivu yoyote, badala ya machozi ya kawaida, damu zinapotitirika ni kitu cha kushangaza" alisema mwanamke huyo.

Viongozi wa dini wa India wanadai kwamba mwanamke huyo ni miujiza toka Mungu.

Monday, November 16, 2009

JOSE MTAMBO NDANI YA ONE LOVE MWANZA


Find more videos like this on G5 world

KAAAAAAA HUMOOOOOO

BONGO FLEVA FIESTA FREESTYLE MC SHUJAA ILIKISANUA MBAYA MJENGONI


mzuka ukipanda habari ndio hiii mtu mzima ncha kali mc of that day

mr climax in the house

The king himself Lusajo jackson ambae ndie aliekuwa mshindi wa Bongo fleva frestyle mc shujaa mwaka 2008 akitema madini kumbattle mkali wa freestyle Mr climax na kumtupa kuleee

An upcoming artist na mmoja kati ya watashambulia jukwaa la fiesta mwaka 2009 muite Bekha Tittle akiperfom ngoma yake (mwendo wa maringo)

Director mwenyewe nilikuwepo kumake sure kila kitu kinaenda sawa. kulia ni producer Lamar na kushoto ni Young D

Mteganda akishow love na Baghdaa baada ya kumtupa kule Baghdad na kuingia fainali

Camera man kutoka clouds tv (Kabezi) akichukuwa matukio kwa ajili ya clouds tv

Majaji waliokuwa wakiendesha show nzima kuwatafuta wakali wawili watakaowakilisha kwenye fainali ndani ya fiesta one love 2009. kushoto ni Saigon pamoja na dj steve b Dj skills

Baghdad kulia akiwa na X dizzo wakisubiri time yao ya kubattle

Moo myama akichanana na Sticky yicky

Adam mchovu a.k.a Brother from another mother akiwa live na radio ya watu na huyo mwingine ni Dj aron

Hawa ndio wawakilishi wa camp za kula raha na burudani pamoja na energy ya kushangilia waliojichukulia tickets 20 kila camp pamoja na zawadi kibao za fiesta one love. camp hizo ni Dar mob kutoka makumbusho, Wabishi camp kutoka kiwalani, Wadon town kutoka kigogo mbuyuni, Mishen not complete kutoka kigogo na The swaga brothers kutoka kigogo

G NAKO NDANI YA CHIZIKA BASH IJUMAA



g nako akiwa na bou nako

mtu mzima niki wa pili
Gnako na Nick wa pili walikuwa ndani ya chizika bash ijumaa ya tarehe 13,waliwapa wa2 mpango mzima yaani show nzito licha ya tanesco kufanya vioja vyao mara kadhaa machizi wakiwa jukwaani hivo kupelekea watu kukatishiwa stim walizolipia...mzuka ulirudi majenereta yalipoamshwa na kazi ikaendelea kama kawa!...kwa waliohudhuria,ukweli ni kwamba hiphop aint dead asee!..

Friday, November 13, 2009

Thursday, November 12, 2009

KAMA SIJAELEWA HIVI .......


mkono wa mwanadada nakaaya sumari na tatoo ya ukweli ikisomeka jina la mchizi kutoka kundi la dead prezz M I ambae miezi kadhaa iliyopita alimuingeji



lakini kwa sasa tatoo hiyo inasomeka hivi (n na ramani ya africa) ile ( 1 ) ikiwa imefutiliwa mbali, hapa ndipo maswali yakifatiwa na mshangao mkubwa yanajaa akilini mwangu sasa sielewi!!!!!!!!kama weiye wafahamu tupe maoni yako mazee.

Wednesday, November 11, 2009

HASHEEM THABIT AVUNJIKA TAYA



Mchezaji wa kati wa timu ya Memphis Grizzlies Hasheem Thabeet amevunjika taya lake la chini siku ya jana, alipokuwa akichezea na timu yake wakiminyana na Portland Trail Blazers, mchezo amabo ulimalizika kwa Blazers kutoka na ushindi wa pointi 93 kwa 79.

Hii sasa inamaanisha kuwa Hasheem hatokuwemo kwenye msafara wa timu yake ya Grizzlies itakapokuwa ikienda kucheza na Houston Rockets usiku wa leo.

Hata hivyo habari si mbaya sana za kuumia kwake kwani baada ya uchunguzi wa madaktari imefahamika kuwa, hatohitaji upasuaji, ili kutibu maumivu na wakasema anatarajiwa awe amepona si muda mrefu sana kuanzia sasa, na ni wazi kuwa hii ni taarifa njema ambayo Thabeet atakuwa amefurahishwa nayo, timu yake na Watanzania kwa ujumla.

Tuesday, November 10, 2009

CHEKI NA VIDEO YA DIAMOND/ KAMWAMBIE


diamond ni mmoja kati ya wasanii wapya wanaotarajiwa kufanya vizuri sana siku za mbele ni single yake ya kwanza na inafanya vizuri sana katika upande wa video kupitia boda2boda ya tbc 1 inaitwa kamwambie.BIBI UNAEMUONA HAPO MWISHONI NI BIBI YAKE NA DIAMOND NA AMEFARIKI JUMAMOSI YA TAREHE 7/11/2009. MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI... AMEN

IBUA FILMS STAR TANZANIA YAHAMIA MWANZA


majaji wakishoo love na madeni kutoka a-town

Baada ya mchakato mzima wa kuibua vipaji vya wasanii chipukizi wa maigizo yaani IBUA Film Star Tanzania kuanzia Arusha, zoezi zima linahamia Mwanza katika Nyanza Shule ya msingi iliyopo Balewa Road tarehe 14 na 15 Novemba kabla ya kuhamia Dodoma.

Chipukizi waliofanikiwa kuiwakilisha mkoa wa Arusha ni pamoja na Salum Ahmed Shafii, Pauline Edward Munisi, Michael Elias Mrema, Mbara Meena na Enhard Haruna. Kutokana na mwamko mkubwa wa wasanii chipukizi, fomu za kujiunga na shindano la IBUA Film Star Tanzania zinaendelea kutolewa maeneo mbali mbali na mikoa husika. Hii ni kuwawezesha wasanii chipukizi
majaji akishow love na washirik

kupata nafasi ya kuonyesha uwezo wao ya kuendeleza vipaji vyao na kuviacha vikipotea kwa kukosa njia ya kuvikuza. Usaili wa mikoani utaandaliwa vipindi maalum na kuonyeshwa kupitia mojawapo ya runinga hapa nchini.

Taasisi ya YEC Production, inayojihusisha na kukuza na kuibua vipaji kwa vijana katika ulingo wa filamu nchini, imegundua njia pekee ya kuibua vipaji hivyo na kuviokoa visipotee kwa kuanzisha shindano maalum la kusaka vipaji. Washiriki wataonyeshwa kwenye runinga kupitia kipindi maalum ambapo watazamaji watahusishwa kumpata staa halisi wa filamu Tanzania.

Mbali na kuviendeleza vipaji vyao pia washiriki watapata mafunzo katika nyanja zote kuanzia za uandishi wa muongozo (scripting) hadi uigizaji bora na kuwawezesha kufikia malengo yao.

Vigezo vilivyotumika katika kumsaka msanii huyo chipukizi ni kuwa na umri wa miaka 16 ikiwa ni pamoja na uelewa. Hata kutokuonekana katika tamthilia au sinema ya aina fulani hapa nchini hicho pia ni kigezo kimojawapo ambacho ni kizuri, kwani vijana wanaochipukia ndiyo wanahitaji msaada mkubwa katika kuibuliwa vipaji, tofauti na wakongwe ambao tayari wamejitangaza.

YEC, imeahidi kuyaangalia matatizo yanayowakabili wasanii kwa kina na kuahidi kutoyarudia, kama yanavyofanywa na baadhi ya wasanii wakongwe, ndiyo maana wameamua kuingia mikataba ya mwaka mmoja na washindi watakaofika kumi bora, ili kuliepuka tatizo hilo.

ALBUM YA NGWEA KWENYE KONA KUINGIA SOKONI


album ya mtu mzima mwenye sur name ya freestyle Ngwea,a.k.a mimi inayoitwa NGE (nyota yake) ikiwa na mwaka aliozaliwa 1982 kwenye poster unayoiona hapo juu itaingia sokoni sio muda mrefu.

MKALI WA ZOUK KUTOKA IRINGA



WAKALI WA ZOUK TANZANIA MPO TAYARI? Msanii mpya wa mahadhi ya ZOUK
anayekuja juu kwa kasi ya ajabu zaidi ya kimbunga cha TSUNAMI,ni zao
jipya kutoka Nyanda Za Juu Kusini nazungumzia wilaya ya Njombe ndani
ya mkoa wa IRINGA ni msanii anayejulikana kwa jina la kisanii AMANI
WETU jina lake halisi ni AMANI SAID KILLO,anaingia kwenye ulingo wa
Zouk akijitambulisha na wimbo wake mpya uitwao 'MAPENZI NI ZAWADI'
ikiwa ndio maandalizi ya Album yake ya kwanza itakayo kwenda kwa jina
la MOYO FICHO LA SIRI.mpaka sasa amesharekodi nyimbo nne katika studio
ya SOUND POWER chini ya Producer B jayzee(THE PROVIDER) studio hiyo
ipo Njombe mjini.Mpaka sasa kazi ambazo amesharekodi ni pamoja na
MAPENZI NI ZAWADI,RAFIKI,MOYO FICHO LA SIRI na WAUZA SURA na kazi
nyingine mpya inayopikwa jikoni kwasasa inaitwa NIMEMPATA,Hivyo
anaomba wapenzi wa muziki wa Zouk wakae tayari kwani mwanzoni mwa
mwaka 2010 album yake itakuwa sokoni

Monday, November 9, 2009

BABA MZAZI WA MANDOJO AMEFARIKI DUNIA


baba mzazi wa mandojo wakwanza kutoka kushoto anaejulikana kama francis michael ongoso amefariki dunia leo hii na mazishi yatafanyika kwao Manyoni Singida.MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEM MAHALI PEMA PEPONI,,, AMEN

MAISHA CLUB KWISHAAAA ...YATEKETEA KWA MOTO

sehemu kuu ya burudani Maisha Club iliyopo Masaki jijini Dar leo mnamo majira ya saa saba mchana ilianza kuwaka moto, kwa taarifa zilizopatikana kutoka kwa mashuhuda wamesema kuwa kulikuwapo na ukarabati uliokuwa unaendelea wa vipupwe (AC), kwa bahati mbaya wakati wa ukarabati huo mojawapo ikalipuka kutokana na nyaya zake kugusana, na baadaye moto mkubwa ukazuka katika jengo hilo, imeelezwa kuwa taarifa zilifika kwa watu wa zima moto lakini hawakuwahi kuuzima moto huo kwa haraka kwani kwa asilimia kubwa vitu vilivyokuwemo vilikuwe vimekwishateketea.

hii ndio ilikuwa sehemu ya kuingilia maishani

sura ya mbele ya club maisha kulia ndipo swiming pool ilipo

maisha club inavyoonekana baada ya kuwaka moto