
Ofisi ya Bunge imesema haijapata barua yoyote kuhusu kuvuliwa uanachama kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema).
Kauli ya hiyo ya Bunge imekuja siku moja baada ya Chama cha
 Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kutangaza kumvua uanachama Zitto, 
ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za 
Serikali (PAC).
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es 
Salaam, Katibu wa
Bunge, Dk. Thomas Kashililah, alisema kutokana na hali hiyo, Zitto bado ni mbunge halali wa Kigoma Kaskazini na kwamba anapaswa kuendelea na shughuli zake kwa mujibu wa sheria.
Bunge, Dk. Thomas Kashililah, alisema kutokana na hali hiyo, Zitto bado ni mbunge halali wa Kigoma Kaskazini na kwamba anapaswa kuendelea na shughuli zake kwa mujibu wa sheria.
Dk Thomas Kashililah, amebainisha kuwa endapo Bunge 
litapata taarifa rasmi ya Chadema kumvua uanachama Zitto, lazima Bunge 
hilo lifanye kwanza uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili ndipo litoe 
uamuzi.
Pia amesema sakata la mbunge wa Bunge hilo kuvuliwa 
uanachama na chama chake si la kwanza, kwani tayari kuna mbunge 
aliyevuliwa uanachama na chama chake lakini Bunge hilo halikumvua 
uanachama wake baada ya kumaliza uchunguzi wake. Hata hivyo hakumtaja 
mbunge huyo.
“Utaratibu ulivyo, chama huliandikia Bunge kuhusu kumvua
 uanachama mbunge na Bunge kabla ya uamuzi wowote hufuatilia kwanza 
sababu za kuvuliwa uanachama huo, ili kujiridhisha kama zilikuwa halali 
au la,” alisema Kashililah.
Alisema baada ya hapo Bunge hilo huwasiliana na Msajili wa 
Vyama vya Siasa ili ofisi hiyo ya msajili iweze kupitia Katiba ya chama 
husika na kupitia sababu za chama husika zinazoweza kumvua uanachama 
mwanachama wake na kama kweli zimekiukwa.
“Baada ya suala hilo kupelekwa kwa msajili wa vyama vya 
siasa, Spika wa Bunge, hutoa uamuzi baada ya kuchunguza na uamuzi huo, 
hupelekwa kwa Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) kwa ajili ya kufanyiwa 
kazi zaidi,”alisisitiza.
Aidha alisisitiza: “Si lazima Spika akubaliane na uamuzi
 wa kutengua ubunge wa mbunge husika kwani kama haikuwa halali kwa 
mbunge huyo kuvuliwa uanachama, Spika hubatilisha uamuzi wake wa kumvua 
ubunge mhusika,” alisema.
Alisema Spika Anne Makinda katika kipindi chake alishawahi 
kutoa uamuzi wa kubatilisha mbunge fulani kuvuliwa ubunge hata baada ya 
chama chake kumvua uanachama.
Akizungumzia suala hilo, Zitto, alisema kwa upande wake 
bado ni mbunge na anaendelea na kazi yake ya Uenyekiti wa Kamati ya 
Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC) hadi pale atakapopatiwa taarifa rasmi
 ya kuvuliwa uanachama na ubunge wake.
“Naendelea na kazi kama vile hakuna kilichotokea, sina 
taarifa yoyote ya kuvuliwa uanachama wangu wala ubunge, habari hizi 
nimezisikia kwenye vyombo vya habari, sijaitwa na Mahakama kuambiwa 
kinachoendelea,”alisema Zitto.
Alisema kwa sasa anaendelea kuongoza kamati hiyo na jana 
alikutana na menejimenti ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), leo 
kamati yake inatarajia kukutana na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), pia 
watakutana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mwanasheria Mkuu 
kuhusu mapato ya akaunti za madini.
Aidha alisema pamoja na kuendelea kama kawaida na shughuli 
zake za kibunge bungeni, pia anatarajia kesho kwenda Kigoma kwa ajili ya
 shughuli za maendeleo jimboni kwake, kabla ya kuhudhuria vikao vya 
Bunge vinavyotarajiwa kuanza rasmi Machi 17, mwaka huu.
Alisema kwa upande wake, anachukulia suala hilo kama 
changamoto ambayo inazidi kumkuza na kumkomaza katika medani za siasa 
nchini na duniani kote.
Kwa upande wake, Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene 
alisema chama hicho kinajitahidi kulifanyia kazi suala hilo kwa 
kuzingatia sheria na taratibu zote, ikiwemo kuandaa na kuiwasilisha 
wakati wowote barua inayomvua uanachama Zitto, ili suala hilo lifanyiwe 
uamuzi mapema.
“Kwa sasa suala hili la Zitto limewaingia Watanzania 
wengi, sasa sisi tunataka tulifanyie kazi mapema, ili uamuzi ufanywe 
mapema na suala hili liishe. Kuna mambo mengi ya maana yanahitaji 
kujadiliwa kitaifa kama vile masuala ya uandikishaji katika Daftari la 
Wapiga kura kwa mfumo wa BVR,” alisema.
Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu ambaye juzi 
alitangaza kuwa chama hicho kimemvua uanachama mbunge huyo, jana 
alimwambia mwandishi kuwa, jopo la wanasheria wa chama hicho 
litaifikisha taarifa ya Zitto kuvuliwa uanachama kwa Kamati Kuu ya 
chama ifikapo Mei, mwaka huu.
Alisema, "Kutokana na utaratibu uliopangwa wa Kamati Kuu
 kukutana kila baada ya miezi mitatu, suala la Zitto litasubiri kikao 
kingine cha kawaida cha kamati hiyo kitakachokaa mwezi Mei. Kikao 
kilichopita kilikaa Februari mwaka huu".
Kwa maelezo ya Lissu, baada ya hapo ndipo wataiandikia 
barua Tume ya Uchaguzi (NEC) kuijulisha kuwa Zitto si mwanachama wa 
chama hicho tena au la.
Handsome! Nice post! thank you for your post!
ReplyDeleteTrương Cầm
Beautyful girl at Sakura Beauty Corp
เกมส์ดีๆที่ใครๆก็เลือกเล่น live22 ฟรีเครดิต
ReplyDeletehttps://www.slot4u.com/live22
ดูหนังออนไลน์ ได้ที่ Doonung1234 ฟรี 2020 ระดับ HD 4K หลากหลายเรื่องมากมาย สนุกกับเรื่ิอง Complete Unknown กระชากปมปริศนา (2016)
ReplyDeleteเกมสล็อตออนไลน์ เครดิตฟรี pgslot โบนัส100 slot online
ReplyDeletehttps://www.diigo.com/item/note/7fmkn/vx3j?k=94724a3edf13efc8b271eb32525f60e3
ReplyDeleteเกมสล็อตอออนไลน์ เครดิตฟรี joker123 โบนัส100 เล่นง่ายได้จริงไม่มีโกง เว็บไซด์เกมออนไลน์มหาสนุก
https://www.slot4u.com/joker123
Thank you for all of your work on this web page.
ReplyDeleteสูตรบาคาร่าแม่นๆ
สูตรบาคาร่าแม่นๆ
สูตรบาคาร่าแม่นๆ